Mhubiri 10:15 “Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja, Maana hajui hata njia ya kuuendea mji.” Kama tunavyojua ni wazi kuwa Kila mtu anatamani kuishi mjini kuliko mashambani; Hii ni kwa sababu mjini kuna huduma zote kwa urahisi zaidi, pia ni mahali pa raha kiasi kwamba watu hufanya kazi zao mashambani ili wakaziuze mijini, kadhalika nakufaidi ..
Category : Maswali ya Biblia
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo na libarikiwe sana. Swali: Tunasoma unabii juu ya masihi (katika Isaya 53:12) kwamba atagawiwa sehemu pamoja na Wakuu.. Sasa JE Wakuu hao ni akina nani? Na ni sehemu gani watagawiwa pamoja? Jibu: tusome.. Isaya 53:12 “Kwa hiyo nitamgawia sehemu PAMOJA NA WAKUU, Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari; ..
Swali: Neno la Mungu katika mhubiri 9:16 linasema hekima ya maskini haisikilizwi. JE na sisi tunapaswa kupuuzia mashauri au hekima za watu maskini? Kama si hivyo, basi Hilo andiko Lina maana Gani? Jibu: tusome tena.. Mhubiri 9:16 “Ndipo niliposema, Bora hekima kuliko nguvu; walakini hekima ya maskini hudharauliwa, wala maneno yake hayasikilizwi.” Tunaposoma andiko hilo ..
Shalom, karibu tujifunze Maneno ya Uzima. Isaya 55:13 “Badala ya michongoma utamea MSUNOBARI, Na badala ya mibigili, mhadesi; Jambo hili litakuwa la kumpatia Bwana jina, Litakuwa ishara ya milele isiyokatiliwa mbali.” Misunobari ni miti Jamii ile ile na Mierezi. Na tofauti kati ya miti hii miwili ni kwamba misunobari huwa haiwi mirefu kama Mierezi, na ..
Nakusalimu katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Mithali 27:22 “Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni pamoja na ngano; Upumbavu wake hautamtoka.” Kwanza kabisa tujue maana ya kinu na mtwangio; hivi ni vyombo vinavyotumika kuponda au kusaga nafaka laini kuwa unga mfano mahindi na ngano. Au wakati mwingine mimea migumu kuwa laini mfano kisamvu hupondwa-pondwa ..
Dhabibu za roho ni zipi, zinazotajwa kwenye biblia? 1Petro 2:5 “Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo”. Dhabihu ni sadaka za kuteketezwa hizi zilitolewa katika agano la kale. Hizi sadaka zilikuwa na lengo la kufanya upatanisho wa ..
Biblia inasema katika Yakobo 4:9Kwamba kucheka kwetu kugeuzwe kuwa maombolezo, je Mungu hapendi tuwe tunafurahi? Au maana yake ni nini mstari huu? Maandiko yanasema… Yakobo 4:9 “Huzunikeni na kuomboleza na kulia. Kucheka kwenu na kugeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa hamu”. Kicheko kilicho tajwa hapo ambacho kinapaswa kigeuzwe kuwa maombolezo sio kicheko cha mambo mazuri, kwamba ..
Pitia hapa.. Ezekieli 27:8 “Wakaao Sidoni na Arvadi ndio waliovuta makasia yako; wana wako wenye akili, Ee Tiro, walikuwa ndani yako, ndio WALIOKUWA RUBANI ZAKE”. Marubani tunaowasoma hapo hawakuendesha ndege kama marubani wa sasa hivi kwa sababu kwa wakati huo ndege hazikuwepo. Neno rubani asili yake ni mwana maji na sio mwana anga kama linavyotumika ..
Tusome hapa.. Mathayo 14:23 “Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake. 24 Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; MAANA UPEPO ULIKUWA WA MBISHO. 25 Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari. 26 ..
Shalom, karibu tujifunze biblia, JIBUMwivi na mwizi ni neno moja lenye maana ileile ila ni lugha mbili ambazo zipo katika nyakati mbili tofauti. Biblia imetafsiriwa kwa kiswahili cha zamani kilichoitwa ‘kimvita’ ambacho kina maneno yasiyokuwepo kwa sasa kama vile mwivi na wevi yakimaanisha mwizi na wezi. Hiyo ndiyo sababu hatuwezi kuona neno mwizi na badala ..