SAUTI YA SHUKRANI NI SADAKA MBELE ZA MUNGU. Yona 2:9 “Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani; Nitaziondoa nadhiri zangu. Wokovu hutoka kwa BWANA”. Shalom, mtu wa Mungu karibu tujifunze Neno la Mungu, Taa iongozayo miguu yetu..na mwangaza wa njia zetu…Leo tutajifunza juu ya Kumshukuru Mungu kwa sauti tu. Unaweza usiwe na kitu cha ..
Author : Yonas Kisambu
YONA NDANI YA MERIKEBU Yona 1:5 “Basi wale mabaharia wakaogopa, kila mtu akamwomba mungu wake; nao wakatupa baharini shehena iliyokuwa merikebuni, ili kuupunguza uzito wake. LAKINI YONA ALIKUWA AMESHUKA HATA PANDE ZA NDANI ZA MERIKEBU; AKAJILAZA, AKAPATA USINGIZI”. Yona alikuwa mmoja wa manabii wa Israeli wakati wa utawala wa Yeroboamu Mfalme wa Israeli, ambaye Mungu ..
MTU AKINITUMIKIA NA ANIFUATE Yohana 12:26 “Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu”. Nakusalimu katika jina kuu lipitalo majina yote mbinguni na duniani, jina la YESU KRISTO WA NAZARETHI. Karibu tujifunze maneno yake ya uzima. Watu wengi wanataka kumtumikia Bwana Yesu, lakini hawataki kumfuata. Wanataka wamtumikie ..
JE UNAJUA NI NINI KITATOKEA MUDA MFUPI BAADA YA UNYAKUO? Bwana Yesu Kristo asifiwe. Karibu tujikumbushe mambo ya msingi yatupasayo kufahamu katika nyakati hizi za hatari.. Baada ya Unyakuo kupita maisha yataendelea kama kawaida, lakini kutasikika tetesi tesi kuwa kuna watu wanaripotiwa kupotea katika mazingira yakutatanisha. Hakutakuwa na furugu kama inavyojulikana na wengi kuwa unyakuo ..
JE! UNYAKUO UTAKUWA NI WA SIRI KWA WATU WOTE? Bwana Yesu Kristo asifiwe wateule wa Mungu. Karibu tujifunze maneno matukufu ya Mungu. Ni kweli unyakuo utakuja ghafla kwa watu wengi, lakini kwa wateule wa Mungu (watakatifu) haitakuwa ghafula, bali watakuwa wanafahamu majira na nyakati hatua kwa hatua, Kama haufahamu Biblia ilishatupa mwangaza juu ya suala ..
FAHAMU MADHAIFU ANAYOYATAMBUA MUNGU KWETU. Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe. Mambo mengi yanayoendelea katika ulimwengu wa mwili ni ufunuo wa mambo yanayoendelea katika ulimwengu wa roho..Uhusiano wa Baba na mtoto..ni ufunuo wa Uhusiano wa Baba yetu wa mbinguni na sisi watoto wake tuliopo hapa duniani…Kama Baba mzazi asivyoweza kumdharau mwanawe hata kama afanye jambo ..
USIDANGANYWE NA DHAMBI Waebrania 3:12-13 “Angalieni, ndugu zangu, usiwe katika mmoja wenu moyo mbovu wa kutokuamini, kwa kujitenga na Mungu aliye hai. [13]Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa UDANGANYIFU WA DHAMBI. Dhambi huwa inadanganya, inaweza ikakuahidi kuwa utapata mafanikio baada ya kuiba, baada ya kusema uongo, baada ya ..
HUKUMU IKAWEKWA NA VITABU VIKAFUNGULIWA. Danieli 7:9 “Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mzee wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu zake moto uwakao. [10]Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; ..
KUBALI KUIPOTEZA NAFSI YAKO ILI UIPATE Shalom. Karibu tujifunze hekima ya kiMungu, Neno lake lililo taa ya miguu yetu na mwanga wa njia zetu (Zaburi 119:105). Ukichunguza kwa umakini zaidi jinsi mambo yalivyo, utagundua kuwa hekima ya dunia inavyoenenda ni tofauti kabisa na wakristo wanavyopaswa kuenenda. Ndio maana Bwana Yesu alituambia maneno haya ambayo tunayasoma ..
TABIA YA ROHO MTAKATIFU KWA MWAMINI MPYA. Jina la Bwana wetu Yesu Kristo lisifiwe daima, Ni siku nyingine tena Bwana aliyotupa kwa neema zake na leo tutaangalia tabia za Roho Mtakatifu katika kumtakasa mwamini katika hatua za kwanza. Kumbuka mwamini ni mtu aliyemwamini Bwana Yesu na kuamua kumfuata kweli kweli. (Kwa ufupi mtu aliyezaliwa mara ..