MACHO YAKO YAMETIWA NURU? Biblia inasema katika… Waefeso 1:18 “macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo” Biblia inapozungumzia mioyo..haimaanishi hii mioyo iliyomo ndani ya vifua vyetu inayosukuma damu…hapana bali inazungumzia utu wa ndani ambao ni roho zetu. Hivyo ..
Category : Biblia kwa kina
MAENEO ANAYOJARIBIWA MWAMINI. (Eneo la kwanza analojaribiwa Mwamini.) Shalom nakusalimu katika jina la Mwokozi wetu Yesu Kristo. Wakristo wengi wanaangamia kwa sababu ya kukosa maarifa, ni muhimu sana kuwa maarifa/ufahamu kwa sababu hakuna vita ambayo Mkristo anaweza kushinda ikiwa hana maarifa unless Neema ya Mungu tu isimame. Tupo katika vita na vita vyetu si juu ..
Mavazi ya kujistiri ni yapi? Biblia inatufundisha tuvae mavazi ya kujistiri na kuwa na adabu nzuri. 1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani; [10]bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo ..
IMEANDIKWA. Nakusalimu katika jina la Mwokozi wetu Yesu Kristo Karibu tuyatafakari meneno ya uzima. Ukisoma katika kitabu cha Mathayo ile sura ya nne wakati Yesu anajaribiwa kule jangwani na ibilisi utaona katika kila eneo shetani alipokua akimjaribu Bwana Yesu Bwana Yesu katika sehemu Zote anajibu “IMEANDIKWA“ Watu wengi huwa tunalitumia hili Neno kwa namna ya ..
Je! Udongo umwambie yeye aufinyangaye; Unafanya nini? Isaya 45:9 “Ole wake ashindanaye na Muumba wake! Kigae kimoja katika vigae vya dunia! Je! Udongo umwambie yeye aufinyangaye; Unafanya nini? Au kazi yako, Hana mikono? Udongo unaozungumziwa hapo ni sisi wanadamu, na Mungu ndiye mfinyazi/muumbaji. Yeremia 18:1-6 Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa BWANA, kusema, [2]Ondoka, ..
TEMBEA KATIKA WAKATI WA MUNGU. Shalom mtu wa Mungu, karibu tujifunze maneno ya uzima. Neno la Mungu linasema.. “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu”.(Mhubiri 3:1) Kila kitu Mungu ameiweka katika wakati wake, hivyo ni vizuri kufahamu wakati wa Mungu katika maisha yako ili usijilazimishe kutembea katika wakati wa ..
TOKA KATIKA GEREZA LA DHAMBI Siku zote mtu anayeishi katika dhambi (ambaye hajaokoka), yupo katika kifungo cha uovu. Matendo ya Mitume 8:23 “Kwa maana nakuona u katika uchungu kama nyongo, na tena u katika kifungo cha uovu”. Na kama tunavyojua wafungwa wanafungwa gerezani ili watumikie vifungo vyao. Na kila mtu ana kifungo chake kulingana kosa ..
MTAFAKARINI SANA Waebrania 12:3 ”Maana MTAFAKARINI SANA yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu”. Nakusalimu katika Jina kuu lipitalo majina yote mbinguni na duniani, jina Bwana Yesu Krosto. Karibu tujifunze Neno la Mungu kwa kina. Tumeambiwa “TUMTAFAKARI SANA” huyu YESU tunayemtaja kila siku. Huyu ..
FAHAMU MAPEPO YANAVUTIWA NA NINI KWA MWAMINI? Shalom nakusalimu katika jina la mwokozi wetu karibu tuyatafari maneno ya uzima ya mwokozi wetu Yesu Kristo. Umeshawahi kufikiri ni kwa nini Wakristo wengi wanafanyiwa ukombozi(deliverance) kutoka kwenye vifungo vya adui ilihali hapo awali walikua wameokoka? Hebu tutafakari mstari huu Bwana Yesu anamwambia mwanamke mmoja aliekuwa amekamatwa kwenye ..
TAZAMA MWANA-KONDOO WA MUNGU AICHUKUAYE DHAMBI YA ULIMWENGU. Jina la Bwana na mwokozi wetu, Mkuu wa uzima, Mfalme wa wafalme, Yesu Kristo libarikiwe. Leo tutaangalia ni kwa jinsi gani BWANA YESU alichukua dhambi ya ulimwengu kama Yohana Mbatizaji alivyomnena katika.. Yohana 1:29 “Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, ..